Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Kikwete akutana na mfalme wa Qatar

01/12/2008

JK akiongea na Emir wa f Qatar sheikh Hamad bin Khalifa al Thani hoteli ya Four Seasons jijini Doha leo. JK yuko huko kuhudhuria mkutano wa fedha na maendeleo.

Mtawala wa Qatar, (The Emir His Highness Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani) amesema kuwa wakati umefika kwa nchi za Afrika kubadilisha mawazo kwa kutafuta mitaji ya uwekezaji katika nchi tajiri za Kiarabu, badala ya kuendelea na jadi ya kusaka raslimali za maendeleo katika nchi za Magharibi.

Mtawala huyo wa Qatar pia ametaka hatua zaidi kuchukuliwa ili kuimarisha uhusiano wa kihistoria kati ya nchi yake na Tanzania, akisisitiza kuwa hata muziki, jadi na utamaduni wa nchi hizo mbili vinafanana.

Mtawala huyo ameeleza hayo wakati alipomkaribisha na kufanya mazungumzo na Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye yuko Qatar kuhudhuria mkutano wa kimataifa unaojadili jinsi ya kusaka fedha za kugharimia maendeleo na jinsi ya kukabiliana na matatizo ya sasa katika mfumo wa fedha duniani.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©