Albino United yazawadiwa
06/12/2008

Mtangazaji
wa idhaa ya Kiswahili ya redio Ujerumani (a.k.a Deutche Welle) Aboubakar
Liongo akikabidhi mipira kwa kiongozi wa Albino United. Mipira ambayo
kituo hicho maarufu cha redio jijini Dar es Salaam kimejitolea wakati wa
mazoezi kiwanja cha Ocean Road.

Picha ya
pamoja baada ya makabidhiano katika uwanja wa Ocean Road ambako Albino
United hufanyia mazoezi kila siku. Timu hii inajiandaa kupambana na
kikosi cha haki ya binadamu hapo desemba 10, 2008 katika uwanja wa taifa
katika kusherehekea siku ya haki ya binadamu duniani.
misaada
zaidi inahitajika kwa ajili ya timu hii ya Albino United ikiwa ni pamoja
na viatu vya kuchezea, jezi na pia kofia (za pama), mafuta ya kuzuia
kuungua jua, maji ya kunywa, madawa ya huduma ya kwanza na kadhalika.
Kuwasiliana na Albino United, mpigie mratibu Oskar Haule namba +255 716
040 550.
|