Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Sherehe za Eid-el-hajj Festival 2008 (1429H)

14/12/2008

Baadhi ya Waislamu wanaozungumza Kiswahili wa East London walijumuika pamoja katika kusheherekea sikukuu za kuadhimisha kufaulu kwa nabii Ibrahim (A.S) baada ya kupewa mtihani na Mwenyezi Mungu (S.W) wa kumchinja mwanawe nabii Ismail (A.S) na bila ya kusita wote wawili walikubaliana na uamuzi huo mpaka Mwenyezi Mungu (S.W) alipowashushia kondoo baada ya kuangalia nia waliyokuwa nayo ya kutimiza maamrisho yake (S.W).

Pichani ni Munawwar Mussa, mtoto anayechipukia katika jamii ya Kiswahili mwenye kuonyesha vipaji alivyokuwa navyo, alifungua kwa kusoma Qur'an (suratul Imran aya ya 96 mpaka aya ya 109) na tafsiri yake na kufuatiwa na utenzi wake mbele ya waliohudhuria katika hafla hiyo ya Eid-el-hajj Festival 2008 iliyoandaliwa na Zenjydar Community Association.

Katika kutimiza hafla hiyo, Zenjydar ilialika jumuia zote za karibu za East London kujiunga kwa pamoja katika kusheherekea sikukuu hiyo kubwa na kuweza kutunisha mifuko mbalimbali ya maendeleo ya jumuia hizo. Pichani juu, Ustadh Hafidh Karama akiwakilisha East African Education Foundation akiwa katika meza yake.

Baada ya mwaka wa jana jumuia ya East African Education Foundation na jumuia ya Alnoor CET ya Barking kushiriki kwa pamoja katika hafla ya Eid-el-hajj Festival iliyoandaliwa na Zenjydar tarehe 23/12/2007, mwaka huu sherehe ya Eid-el-hajj iliyoandaliwa na Zenjydar iligongana na sherehe ya Alnoor CET ya Barking kutokana na jumuia zote mbili kukosa ukumbi siku ya Jumamosi ya tarehe 13/12/2008 (wikiendi ya mwanzo ya siku ya Eid-el-adhaa), lakini jumuia zote zimejulishana hali hiyo na wote wamekuwa radhi kuendelea kufanya siku moja kwa nia moja. Aidha, jumuia nyingine alikwa zilikutwa na dharuri ya kutohudhuira katika hafla hiyo.

Nyota nyingine inayochipukia katika jamii ya Kiswahili mtoto Omar Salum (kushoto) akiwa katika mchezo wa kuigiza wa Kiislam, akiwa na muigizaji nyota chipukizi katika jamii ya Kiswahli bwana Farid Nassor (kulia) ambao walionyesha ustadi wao katika mchezo huo wa kuigiza ambao ulisisimua watu kwa majonzi na vicheko ambao ulitungwa na kuendeshwa na bwana Saleh Jaber.

Omar Salum (kulia) na bwana Farid Nassor (kushoto) wakionyesha umahiri wao kwenye steji.

Ana kwa ana bwana Farid Nassor (kulia) ambaye alijulikana kwa jina la "Kikoi" akimueleza jambo Omar Salum (kushoto) ambaye alijulikana kwa jina la "Kibandiko".

Bwana Kikoi (Farid Nassor) akionyesha hisia zake kwa kumueleza jambo rafiki yake bwana Kibandiko (Omar Salum).

Bwana Kibandiko (Omar Salum) akinyosha mikono juu na kusema aliyoyasema kwenye mchezo huo wa kuigiza wa Kiislam.

Bwana Kibandiko (Omar Salum) akionekana akimuuguza rafiki yake bwana Kikoi (Farid Nassor) akiwa chini katika mchezo wa kuigiza wa Kiislam.

Pichani ni waliohudhuria katika sherehe ya Eid-el-hajj Festival 2008, kutoka kulia ni bwana Naher, akifuatiwa na bwana Abdulkareem na mtoto wake Faiz, na kushoto Mheshimiwa bwana Said Suleiman Omar.

Kutoka kulia ni bwana Salum Omar akiwa na Aisha, na kushoto ni Mheshimiwa Ustadh Nassor Haroub (Mwenyekiti wa East African Education Foundation).

Pichani kulia ni bwana Mussa akwa na watoto wake Mundhir na Mahir ambao wakiwa katika mchanganyiko na waototo wenzao waliofika katika hafla ya Eid-el-hajj Festival 2008.

Baadhi ya watoto wengine wakiwa katika viti vyao wakipata chakula cha Urojo ambao ndio kilikuwa chakula maalum cha sherehe hiyo "Special Urojo Evening".

Watoto waliofika katika sherehe hiyo walikuwa katika hali ya urafiki na udugu.

Katika kuhitimisha sherehe ya Eid-el-hajj Festival 2008, Zenjydar Community Association ilijitolea mchango wake wa kukuza mfuko wa kuchangia jumuia ya Alnoor CET ya Barking na jumuia ya East African Education Foundation katika miradi yao kwa kunadisha mnada wa saa ya ukutani ambayo imesanifiwa vizuri kwa sanaa za Kiislam.

Baada ya vuta nikuvute ya mnada huo, hatimaye bwana Omar Khaleef (pichani juu) alishinda saa hiyo na kuweza kuichukua nyumbani kwake. Asilimia Hamsini ya pesa zote zilizopatikana katika mnada huo zitakwenda katika mfuko wa Alnoor CET Barking na Asilimia Hamsini itakwenda kwenye mfuko wa East African Education Foundation.

Hongera bwana Omar Khaleef! Wabillahi Tawfeeq.

Zenjydar Community Association inawatakia wote sikukuu njema ya mwaka 2008 (1429H) na kheri za mwaka mpya 2009 (1430H).

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©