Taifa Stars yaizamisha
Nile Crocodiles ya Sudan 2-1
15/12/2008

Mkereketwa na mmoja wa
viongozi wa kamati ya Saidia Stars Ishinde Dk. Ramadhani Dau naye
alikuwepo toka Sudan na katika msafara ambapo alidanda juu ya gari toka
Eapoti hadi mjini.
Ushindi
wa Taifa Stars ambao iliupata Jumamosi kwenye Uwanja wa Al Hilal jijini
Khartoum, Sudan, dhidi ya wenyeji Nile Crocodiles umefungua ukurasa mpya
wa mpira wa miguu Tanzania kwani ni changamoto kwa michezo mingine kuwa
pale ambapo wahusika wanapotimiza majukumu yao ipasavyo hakuna
kisichowezekana.

Ni wazi
kuwa mafanikio hayo si changamoto kwa wachezaji wa Taifa Stars
watakaokwenda Ivory Coast katika fainali hizo zitakazoshirikisha timu
nane, bali itakuwa vilevile kwa wachezaji chipukizi na wale wanaoinukia
lakini hawafanikiwi kupata nafasi ya kuitwa kwenye timu hiyo.
Pia
tunaupongeza uongozi mpya wa TFF uliochaguliwa katika uchaguzi
uliofanyika Jumapili chini ya Rais Leodegar Tenga na makamu wake wawili
Athuman Nyamlani na Ramadhan Nassib.

Uongozi
huo una changamoto kubwa ya kulinda mafanikio yaliyopatikana na
kutekeleza mengine ambayo hayakufanyika katika awamu iliyopita.
Changamoto hiyo ni kubwa kwa vile wadau wana matumaini makubwa kutoka
kwa safu hiyo mpya.
Lakini
shukrani za pekee ni kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu kwa kuchagua safu
ambayo TASWA tuna imani kuwa ina nia, uwezo na sababu ya kukabidhiwa
majukumu hayo hasa wakati huu ambapo hamasa katika mpira wa miguu hasa
kwa timu ya Taifa imeanza kurudi.

Kocha Marcio Maximo wa Taifa Stars
akionyesha alama ya ushindi wa mabao 2-1 kwa tabasamu kubwa.
|