Shujaa wa mwenge wa Uhuru
kuzikwa leo
24/12/2008

Shujaa aliyepandisha Mwenge wa Uhuru
kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro siku ya mkesha wa uhuru wa
Tanganyika, Disemba 9, 1961 amefariki dunia tarehe 20/12/2008 na kuzikwa
leo kwenye makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.
Nyirenda
alizaliwa Tarehe 2 Februari 1936 Karonga, Malawi, wakati wazazi wake
wakiwa katika likizo ndefu ya Krismasi kutoka Tanganyika. Alisoma shule
ya msingi ya Mchikichini Dar es Salaam na baadae shule za Sekondari za
wanaume za Malangali (mkoani Iringa) na Tabora, hadi 1957.

Baadhi ya waombolezaji
wakisubiri mwili wa marehemu kuletwe kwa mazishi. toka shoto ni mzee
Said El Maamry, Meja mstaafu Kashmir, Hamza Kasongo, George Kritsos na
Kanali mstaafu Julius Mbilinyi. Alietupa mgongo hakuweza kutambulika
mara moja.
|