Bi Mariam ajifungua pacha
watatu
27/12/2008

Pichani ni Bi Mariam Rajab mkazi wa
Mwanayamala 'A' Dar es Salaam, ni miongoni mwa akina dada waliojaaliwa
watoto usiku wa tarehe 24/12/2008. Mariam amejifungua pacha watatu
katika Hospitali ya Mwananyamala na yupo katika mtihani mzito wa juu ya
kuwalea watoto hao watatu ambao mmoja kati yao ni wa kike.
Kwa mujib wa Mariam anasema aliyempa uja
uzito huo alimkana tangu mwanzo na hamjali kwa lolote na familia
anayoishi nayo pia ni maskini. Na tangu amelazwa hapo hakuna yeyote
aliyefika kumjulia hali na anategemea msaada mkubwa wa wauguzi. Anaomba
yeyote aliye na msaada wa aina yoyote kumpunguzia ugumu wa kulea viumbe
hivyo visivyo na hatia. Bi Mariam yupo Dar es Salaam lakini habari za
mawasiliano hazikupatikana.
|