Jihadhari Askari Feki
28/12/2008

Pichani juu ni kijana mmoja aliyekamatwa na
polisi jijini Dar es Salaam akijifanya askari wa jeshi la polisi akiwa
amevalia magwanda kama aonekanavyo pichani, hali imekua mbaya siku hadi
siku kutokana na wimbi kubwa la vibaka wanaovalia nguo sare za jeshi la
polisi wakiwa na nia ya kuwatoa wananchi mbalimbali upepo (Hela).
Katika kikao cha waandishi wa habari
jijini Dar es Salaam na kamanda wa kanda Maalum Afande Suleiman Kova
amewataka wananchi wote kwa ujumla kuwa makini na askari wa aina hii (Matapeli),
na pindi ukimtilia mashaka askari yoyote fanya juu chini Ufike nae
kwenye kituo chochote cha polisi kilicho karibu nawe.
|