Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Mali za ATCL (Air Tanzania) zakamatwa

31/12/2008

Pichani ni Moja ya gari la Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) linaloshikiliwa na Benki ya Stanbic Tanzania, likiwa limeegeshwa katika Makao Makuu ya benki hiyo, Dar es Salaam

Benki ya Stanbic Tanzania Limited, Makao Makuu ya Kinondoni, Dar es Salaam, inayashikilia magari sita ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), baada ya kushindwa kulipa deni la Sh bilioni mbili iliyochukua kama mkopo. Fedha hizo zinazodaiwa kushindwa kulipwa kwa miezi miwili sasa zilikopwa na wafanyakazi wa kampuni kwa mikopo na kutokana na kushindwa kuwalipa mishahara watumishi wake, makato ya kila mwezi yameshindikana kukatwa.

Taarifa zilizopatikana kutoka ATCL na katika benki hiyo jana zilithibitisha kushikiliwa kwa magari matano aina ya Toyota Land Cruiser VX, na gari la sita limekamatwa likiwa mjini Moshi, Kilimanjaro na lilipelekwa katika benki hiyo jana na kufanya idadi ya magari hayo kuwa sita.

Waandishi wa habari walitaka habari zaidi kwa undani, lakini uongozi wa benki uliokuwapo haukuwa tayari kuzungumza kwa madai kuwa msemaji wa benki hiyo yupo likizo.

Aidha, inasemekana ndege za ATCL zimefunguliwa mbawa zake kuanza kazi ya kurusha abiria, lakini wafanyakazi wamekosa mshiko wa mwezi mzima wa Disemba.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©