Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Serikali yapitisha £18 MILIONI kunawirisha kata ya Canning Town

01/11/2008

Serikali ya UK imepitisha £18 milioni kuipatia mamlaka ya bara la Newham kwa madhumuni ya ujenzi wa kunawirisha sura ya kata ya Canning Town, bara la Newham, East London, bara ambalo Olimpik ya 2012 London itakapofanyika.

Moja ya sehemu maalumu ambayo ujenzi huo utaanza kufanyika ni barabara ya A13 ambayo ni barabara kubwa inayounganisha wakazi wa Newham kutoka nje na ndani ya bara la Newham.

Diwani Conor McAuley amesema, hii ni habari nzuri kwasababu barabara kubwa ya A13 na mduara wa Canning Town ndio kitovu cha magari yanayotoka katikati ya London, Custom House na pande zingine ambapo kwa sasa imeshaanza kuonyesha ugumu wa usafiri kupitia hapo kutokana na wingi wa magari yanayotumia njia hiyo. Vilevile itasaidia kuunganisha watu wa Newham ambao wamegawishwa pande mbili (kusini na kaskazini) kwasababu ya barabara hiyo kubwa ya A13.

The London Thames Gateway Development Corporation inafanya kazi pamoja na mamlaka ya bara la Newham katika ujenzi huo ambao wamesanii kuwa na sehemu nzuri za matembezi kwa watu, maduka, nyumba za kisasa na maeneo ya biashara.

Usanii wa kuitoa raundiabauti (roundabout) ya A13 ambayo ipo katika kiungo cha A13 na Barking Road imeshaanza. Raundiabauti hiyo itatolewa na kutakuwa na madaraja ya kuunganisha pande zote mbili kwa waendao kwa miguu na wanaosafiri na vyombo vya usafiri.

Ujenzi huo unatarajiwa kuisha mwezi wa tisa (Septemba) 2011.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©