Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

NEWHAM yawakaribisha wawakilishi wa UAE

03/11/2008

Bara la Newham, East London limewakaribisha wawakilishi 11 (kumi na moja) wa kutoka serikali ya dola za Kiarabu (UAE).

Mualiko huo rasmi, umeandaliwa na SLG (Shared Leadership Group) shirika la kuangalia miundo mbinu ya teknolojia ambayo inaendelezwa kwenye mamlaka za serikali. Wadhamini wa maandalizi hayo na mkutano huo walikuwa ni shirika kubwa duniani (MICROSOFT) ambalo ni baba wa teknolojia za kisasa.

Wawakilishi hao wamefika katika kudurusu na kuangalia vipi serikali za UK zinaendeleza teknolojia yake kwenye sekta za huduma za raia vilevile UAE ikiwa ni moja ya nchi zinaazoongoza katika mambo ya ujenzi duniani, wawakilishi hao watafaidika kuangalia vipi Newham imeandaa katika maendeleo ya kiteknolojia ya ujenzi kwa maandalizi ya Olimpik 2012.

Wawakilishi hao wanatarajiwa kudurusu sehemu mbalimbali za teknolojia na kuchukua teknolojia hiyo nyumbani kwao katika maendeleo mbalimbali ya nchini UAE.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©