Rais-mteule Barack Obama
atembelea White House
11/11/2008

Rais-mteule wa Marekani Barack Obama alizuru White House jana katika
mualiko wa mazungumzo na bwana Bush na matembezi ya kuijua nyumba ambayo
anatarajiwa kuhamia mnamo tarehe 20/01/2009 mara tu atakapoapishwa kuwa
rais wa 44 wa Marekani.

Rais-mteule wa Marekani Barack Obama akiwa na rais George W. Bush katika
ofisi ya rais ya ikulu ya White House ijulikanayo kama "The Oval".

Wakati huo huo, bi Laura Bush alimchukua
(soon to be First Lady) Michelle Obama katika kumuonyesha sehemu
mbalimbali za nyumba ambayo familia ya Obama wanatarajiwa kuhamia.

Wanyaka-sura na washabiki wakiwa pembezoni mwa White House wakivizia
kuwaona Rais na Rais-mteule.

Limuzini ambalo Rais-mteule Barack Obama
na Michelle Obama limewabeba, likionekana likivinjari mtaa wa
Pennsylvania Avenue, Washington D.C. baada ya kutoka White House.
|