![]() |
Your community website |
![]() |
||||||
|
|
|
|||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
NEWS |
||||||||
|
|
||||||||
Universal Studios yaungua moto01/06/2008
Jumba maarufu la filamu duniani, Universal Studios, ambalo limezalisha filamu kubwa kubwa nzuri, limeteketea na moto usiku wa kuamkia leo. Moto huo umeteketeza sehemu tofauti ndani ya jumba hilo ikiwemo sehemu inayowakilisha filamu maarufu ya 'Back to the Future" na vilevile sanamu kubwa la King Kong. Moshi wa moto huo ulitanda na kuonekana mji mzima wa Hollywood, Los Angeles. Wanazimamoto 400 walikuwa katika kupigana na moto huo ambao mwisho wameweza kufanikiwa. Inasemekana, karibu video 50,000 zilizohifadhiwa humo zimeungua. Na bahati mikanda ya filamu nyingine ilipona chupu chupu kwa kuwa ilikuwa ndani ya kabati la chuma. Lakini, Rais wa Universal Studios, Ron Meyer amesema, mikanda yote ambayo imeungua, ina kopi zake ambazo zimehifadhiwa sehemu nyingine kuepukana na hali kama hiyo kutokea. Katika moto huo, hakuna majeruhi wala mtu aliyepatwa na moto huo. Ukubwa wa uwanja wa Universal Studios unafika eka 230.
|
||||||||
|
Custom Search
|
||||||||
|
|
|
|||||||
|
©
www.zenjydar.co.uk - Since 2007 |
|
||||||||