![]() |
Your community website |
![]() |
||||||
|
|
|
|||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
NEWS |
||||||||
|
|
||||||||
Jengo laporomoka - Dar es Salaam21/06/2008
Leo hii jengo moja lililopo makutano ya mtaa wa Zanaki/kisutu limeporomoka kwa kile kinachohisiwa kuwa ujenzi usio makini. Inasemekana jengo hilo ambalo bado lilikuwa likiendelea na ujenzi lilikuwa limeshafikia ghorofa kumi kabla ya kuporomoka lote.
Habari ambazo bado hazijathibitishwa wakati uchunguzi ukiendelea zinasema kuwa baadhi ya mafundi waliokuwa wanalijenga jengo hilo ambao bado idadi yake haijajulikana wamefukiwa na hicho kifusi.
Wapita njia wakiwa karibu na eneo ambako jengo la ghorofa kumi lililokuwa linajengwa lilipobomoka lote leo.
Watu wanne wameopolewa na kukimbizwa hospitali. Habari za awali ambazo hazijathibitishwa bado zinasema wanasadikiwa kufa baada ya kufunikwa na kifusi cha jengo hilo.
Inasemekana watu hao wanne walikuwa ndani ya nyumba ya ghorofa tatu iliyo jirani na hilo ghorofa, ambapo baada ya kuangukiwa na kifusi wakawa wamenasa ndani. Hadi milango ya saa kumi watu watatu walikuwa wameshatolewa, na juhudi za kumpata aliyesalia ama waliosalia zinaendelea. Pichani juu, Mwanazimamoto akijaribu kuangalia dalili za majeruhi.
|
||||||||
|
Custom Search
|
||||||||
|
|
|
|||||||
|
©
www.zenjydar.co.uk - Since 2007 |
|
||||||||