Mount Kilimanjaro

 

 

 

Your community website

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

David Beckham kuupanda mlima wa Kilimanjaro

19/05/2008

Mchezaji mpira wa miguu maarufu duniani David Beckham (33) amejiandaa kuupanda mlima mkubwa wa Afrika wa Kilimanjaro ambao upo Tanzania, katika mpango wa kujaza mfuko wa kusaidia watoto ambao umeandaliwa na UNICEF.

Katika mpango huo, akiwa pamoja nae ni muimbaji mashuhuri BONO wa bendi ya muziki ya U2. Katika safari hiyo, BONO atakuwa akisaidia kujaza mfuko wa kusaidia watu wenye Ukimwi (HIV/AIDS).

Inasemekana kuwa, kutokana na urefu wa mlima wa Kilimanjaro ambao una urefu wa futi 19,340, kwa David Beckham itakuwa kazi si ndogo lakini kasema yeye mwenyewe kuwa atajitahidi kufika katika kilele cha mlima huo.

Siku maalum bado haijapangwa kwasababu ya Beckham kuzingwa na kazi za timu yake ya Marekani, LA Galaxy.

Inasemekana itawachukuwa siku 6 kuupanda mlima huo. Beckham kasema, kamchagua BONO kwenda nae kwenye safari hiyo kwasababu BONO ni mtu ambaye mwenye ushawishi mkubwa wa kumfanya yeye aupande mlima huo.

Vilevile, inasemekana golikipa wa timu ya West Ham United, Robert Green (pichani) atakuwa nao pamoja katika safari hiyo. Robert Green atakuwa akisaidia kujaza mfuko wa African Medical Research Foundation.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
Events Calendar
News Archive 2008
News Archive 2007

External Links

Alnoor CET
TZ Embassy UK
TZ's Community UK

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©