Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Baraza la Eid - London 2008

11/10/2008

Kutoka kushoto: Ustadh Makoe, Maalim Abdallah (Mwenyekiti wa ZAWA), Idris Zahran (Ofisa wa habari na mawasiliano Ubalozini UK), Mohammed Zahran (Katibu wa East African Education), Saleh Jaber (Mwenyekiti wa Zenjydar Community Association), Ustadh Issa, Ustadh Khamis Faki (Mwenyekiti msaidizi East African Education Foundation), Salum Abdallah na wajumbe wengine waliohudhuria katika hafla ya baraza la Eid London 2008.

Kutoka kushoto: Bwana Idris Zahran, Abuu Faraj (Mwenyekiti TZUK Association), Saleh Jaber (Mwenyekiti Zenjydar Community Association), Ustadh Nassor Haroub (Mwenyekiti East African Education Foundation) na Abdallah Maka.

Habari Kamili:

Baadhi ya jumuia za East London zilihudhuria kwenye baraza la Eid ambalo limefanyika tarehe 11/10/2008. Baraza la Eid limeandaliwa na jumuia ya ZAWA ikishirikiana na East African Education Foundation na TZUK Association na Ubalozi wa Tanzania nchini UK.

Hii ni mara ya pili baraza la Eid kufanyika tangu mwaka 2007 na kusimamiwa rasmi na Maalim Abdallah.

Katika hafla hiyo, mgeni wa heshima bwana Idris Zahran ambaye aliwakilisha Ubalozi wa Tanzania nchini UK alipata fursa ya kukaribisha wote waliohudhuria na kuleta salamu za Mheshimiwa balozi Mwanaidi Maajar Sinare za Eid Mubarak.

Vilevile bwana Idris alisema, Mheshimiwa balozi anaanzisha mpango wa kukutana na wote wenye jambo lolote ambalo wangependelea kuongelea na Mheshimiwa katika kuleta maendeleo. Mpango huo ambao utakuwa kila siku ya Alhamisi, itakuwa ni siku maalumu kwa yoyote atakayependelea kukutana na mheshimiwa balozi Mwanaidi Maajar.

Picha na Ustadh Khalfan kwa niaba ya Zenjydar Community Association.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©