Bara la NEWHAM kupambana na
madereva hewa
12/10/2008

Bara la Newham ikishirikiana na
Metropolitan Police wameunda kikosi cha kupambana na madereva hewa (madereva
ambao wanaendesha gari bila ya Leseni au bila ya Bima (Insurance).
Kikosi hicho ambacho kinaitwa "Operation
Reclaim" kimezinduliwa rasmi na Diwani Ian Corbett pamoja na Kamanda wa
Polisi wa Newham, Simon Letchford, baada ya matayarisho yaliyoandaliwa
katika kituo cha Polisi cha Forest Gate, Newham.
Operesheni hiyo itakuwa inakamata mitaani
na barabarani magari na madereva ambao hawana Bima au Leseni.
Kamanda Letchford ametoa onyo kali akisema,
"Operation Reclaim" ni nguvu ambayo inawapa Polisi kusimamisha magari
ambayo hayana Bima kwa kutumia vyombo maalum ambavyo vimo ndani ya gari
za Polisi. Mara tu gari itakapokamatwa baada ya kutambulika kuwa haina
Bima, Polisi watamtoza dereva faini £300.00 hapo hapo kwa kumpa tiketi
na kuchukuliwa gari yake hapo hapo.
Dereva anatakiwa akomboe gari yake kwa
kulipa faini hiyo na kuonyesha Bima mpya ndani ya siku zisizozidi 14
baada ya tukio. Ikiwa siku 14 zitapita na gari haijakombolewa, gari hiyo
itapondwa na mashine maalum au itauzwa kwenye mnada.
Operesheni hiyo iliwekwa kwenye majaribio
mwezi wa tisa (Septemba) mwaka huu na Polisi walifanikiwa kukamata
magari 336 ambayo hayana Bima (Insurance).
Polisi wamesema, wanaamini katika bara la
Newham peke yake, hivi sasa kuna magari yasiyopungua 20,000 mpaka 30,000
ambayo hayana Bima.
|