Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Maajabu ya Pete - Dar es Salaam

16/10/2008

OMARI HAMISI, 28, ni kijana aliyekumbwa na balaa la pete kung'ang'ania vidoleni. Kisa chake kinaendelea kuleta msisimko mkubwa baada ya yeye mwenyewe kueleza bayana kwamba tangu avae pete hizo, hana amani kabisa.

Akiongea na waandishi wa habari, Omari amesema, usiku anapokuwa usingizini hupatwa na hali isiyo ya kawaida. Anasema hali hiyo ya ajabu haikuwahi kumpata kabla ya kuokota pete hizo na kuziweka vidoleni mwake. Amesema hali hiyo imekuwa ikimtokea kwa miaka mitatu sasa tangu alipovaa pete hizo.

Omari amesema, "Tangu nizivae miaka mitatu iliyopita, sikuwahi kuzivua, usiku huwa napatwa na hali nisiyoielewa ambayo kabla ya kuzipata pete hizo sikuwa na hali hiyo".

Wakati Omar mwenyewe anaeleza hayo, Mtabiri maarufu katika nchi za Afika Mashariki, Sheikh Yahya Hussein amejitokeza na kutoa maelezo aliyodai kuwa yataokoa maisha ya kijana huyo ambaye hadi sasa amelazwa katika Taasisi ya Mifupa (MOI) na madaktari wanahaha kutafuta namna ya kumsaidia.

Sheikh Yahya amesema, kama kitendo cha pete hizo kung'ang'ania vidoleni kinahusiana na mambo ya kishirikina, basi kinachotakiwa kufanywa ni kumenya vitunguu thumu, kuviponda ponda na kisha kufukiza huku moshi wake ukielekea kwenye vidole hivyo. Amesema iwapo pete hizo ni za majini basi yatatimuka na madaktari wataweza kufanikiwa kuzitoa kwa kuzikata bila matatizo.

Sheikh Yahya amesema, "Kuna majini huwa yanatupa pete na mtu anapookota basi anaweza kupata matatizo kama hayo".

Ameongeza kuwa iwapo zoezi hilo la kitunguu thumu halitafanikiwa, basi ni budi zitafutwe njia nyingine za kumsaidia kijana huyo.

"...siku ya kwanza tulianza kazi ya kuondoa pete zile kwa kutumia sabuni na mafuta, lakini ilishindikana baada ya kuonekana kuwa ngumu kiasi cha kutisha", alisema mmoja wa wauguzi ambaye hakutaka jina lake litajwe.

Hata hivyo, madaktari hawakuishia hapo kwani waliamuru apelekwe katika chumba maalum chenye vifaa vya kuondolea vyuma mwilini, huko ndipo maajabu ya pete hizo yalipoanza kuonekana.

Inasemekana kila walipozigusa kwa mashine hiyo kwa nia ya kuzikata, pete hizo zilitoa cheche za moto ambao ulikuwa ukimuunguza mgonjwa huyo. Hata hivyo, alipoulizwa Afisa Uhusiano wa MOI, juu ya sakata hilo alisema, mgonjwa huyo bado anaendelea kulazwa hospitalini hapo wakati madaktari wanaendelea kufikiria njia ya kuondoa pete hizo ambazo zimesababisha vidole vyake kuanza kuvimba.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©