Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Gari yapiga mbizi Kivukoni - Dar es Salaam

18/10/2008

Askari wa kituo kidogo cha feri wakila doria sehemu lilipotumbukia na kuzama gari aina ya Canter, feri, kivukoni, huku MV Kigamboni ikila mzigo na kufanya safari zake za Kigamboni na kurudi kama kawaida. Chini ni wapiga mbizi wakiwa katika harakati za kulifunga kamba gari hilo.

Gari aina ya Canter limetumbukia baada ya kushindwa kupandisha kimlima cha kutokea kwenye Pantoni upande wa Posta.

Hakuna mtu alilyedhurika na ajali hiyo. Dereva ambaye alikuwa peke yake wakati akitoka kwenye Pantoni, aliamua kuruka baada ya kuona gari imegoma kusimama licha ya kuweka kigogo na utingo wake aliyekuwa nje ya gari.

Juhudi za kulitoa gari hilo katika maji zilishughulikiwa ambapo Wazamiamaji walikuwa wakipiga mbizi kulifunga kamba kabla ya kuliopoa. Inasemekana walifanikiwa kulitoa gari hilo kwa usalama, lakini bado usalama wa kivukoni unahitaji mtazamo wa karibu kwani inasemekana hali kama hizo kutokea si mara ya kwanza.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©