Kadi za wageni wanaoishi
nchini UK
20/10/2008

Hatimaye, Serikali imezindua kadi mpya za
wakazi au wageni ambao si raia wa UK ambao wanaishi nchini UK kwa
madhumuni mbalimbali.
Kadi hizo ambazo zinaitwa "Biometric Cards"
zitatolewa katika wimbi la kwanza katika mwezi wa kumi na moja Novemba
2008, kwa Wanafunzi ambao si raia wa UK lakini wanaishi nchini UK ambao
pia si raia wa nchi zilizoungana za Ulaya (European Union) na zitatolewa
kwa wale ambao wana Viza ya ndoa.
Waziri wa mambo ya ndani bi Jacqui Smith
amesema, Kadi hizo zitasaidia kurahisisha kumtambua mwenye kadi kirahisi
kuwa ni yeye anayemiliki kadi hiyo ambayo itakuwa na habari zote za
mwenye kumiliki kadi ikiwamo hali yake ya makazi ya nchini UK.
Ameongeza akisema, kadi hizo zitasaidia
wale ambao wamo nchini si kihalali kutambulika kirahisi popote
watakapoenda na kutokufaidika na misaada (benefits) ambayo ni ya raia wa
UK.
Kadi hiyo ambayo itatolewa badala ya
karatasi na muhuri ambazo zilizokuwa zikitolewa hapo mwanzoni, zitakuwa
na jina la mwenye kadi, picha yake, uraia wake, vipi anakaa nchini na
alama ya vidole viwili (fingerprints).
|