Sherehe za tunuku ya
Kamisheni Maafisa
21/10/2008

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania
Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na mgeni wake Rais wa Botswana Lt.
Gen. Seretse Khama Ian Khama wakati wa sherehe za kuwatunuku kamisheni
maafisa wa jeshi katika chuo cha jeshi Monduli leo. Jumla ya wanafunzi
22 kutoka Botswana walikuwa miongoni mwa maafisa wapya waliohitimu leo.
Rais Khama aliwasili juzi katika ziara ya kikazi ya siku mbili nchini.

Amiri Jeshi Mkuu JK akikagua gwaride la
heshima wakati wa sherehe za kuwatunuku kamisheni maafisa wa jeshi
katika chuo cha jeshi Monduli leo. Jumla ya wanafunzi 22 kutoka Botswana
walikuwa miongoni mqwa maafisa wapya waliohitimu leo.

Amiri jeshi mkuu JK akimpongeza na
kumzawadia Mwanafunzi bora katika mafunzo ya maafisa wa jeshi Luteni Usu
Israel Ibrahim Mwashala, wakati wa sherehe za kuwatunuku maafisa wapya
wa jeshi waliohitimu mafunzo ya mwaka mmoja katika chuo cha jeshi TMA
kilichipo Monduli, mkoni Arusha.
|