URAFIKI
23/10/2008

Balozi msaidizi wa Tanzania nchini UK,
bwana Chabaka Kilumanga (kushoto) akipokea kwa tabasamu la bashasha
sanaa ya picha ya kuchorwa inayogusia mila na utamaduni wa Tanzania
kutoka kwa bwana Andrew Marshall, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa (District
Commissioner) wa Tarime mwaka 1948 wakati Tanzania ilipokuwa katika
ukoloni wa Great Britain na ikijulikana kama (Tanganyika) miaka hiyo.
Picha hiyo tangu balozi wa kwanza nchini UK
baada ya uhuru wa Tanganyika, bwana Sam Ntiro, ilitolewa rasmi kwa
balozi msaidizi bwana Chabaka Kilumanga nyumbani kwa bwana Andrew
Marshall mjini Bath, UK, Alhamisi iliyopita tarehe 16/10/2008
Bwana Kilumanga alitoa shukran za dhati kwa
bwana Marshall, na kuahidi kuitundika picha hiyo ndani ya chumba kimoja
wapo kilichopo ubalozini UK ili wageni wajapo waone uhusiano mkubwa wa
kihistoria unaotoka mbali kati ya Tanzania na United Kingdom.
|