Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Yanga  yaicharaza Simba 1-0

26/10/2008

Mchezaji wa Yanga Ben Mwalala akipachika bao wavuni huku kipa wa Simba Amani Simba akiuangalia bila kufanya lolote katika mchezo wa Ligi Kuu uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Matokeo ya mechi hiyo: YANGA 1 - SIMBA 0.

Uimara wa kipa Mzungu, Obren Curkovic wa Yanga, pamoja na kuwa na vurugu, imani za kishirikina na matukio yakiwamo ya mashabiki kurusha uwanjani chupa za maji, na kadhalika... ni baadhi ya matukio ambayo yalitawala mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyomaliza karibu miaka minane ya ubabe wa Simba dhidi ya Yanga.

Katika mchezo huo ambao ulikuwa gumzo na ubishi mkubwa miongoni mwa mashabiki,Yanga imefaulu kushinda kwa bao 1-0 katika Uwanja Mkuu wa Taifa,Dar es Salaam.

Mchezo huo uliokuwa wenye ushindani, ufundi mkubwa kulinganisha na mechi nyingine zilizohusishwa katika ligi hiyo, mwishowe Yanga walipata bao dakika ya 15 kupitia kwa Ben Mwalala baada ya kupokea pasi ya Boniface Ambani ambaye aliwatoroka mabeki wa Simba na kutingisha wavu.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©