Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Kivukoni kuwa mambo mkeka

25/09/2008

UJENZI wa kivuko kipya cha Kigamboni utakamilika katikati ya mwezi ujao na kuanza kutoa huduma za usafishaji wa abiria na mizigo kati ya Feri Magogoni na Kigamboni, Dar es Salaam.

Hatua hiyo inatokana na kukamilika kwa ujenzi kivuko hicho kwa kiwango cha asilimia 95. Kauli hiyo ilitolewa leo hapa Dar na Meneja Mwendeshaji, Fuad Saadun, kutoka Kampuni ya Ujerumani ya Neue Ruhrorter Schiffswerft GMBH wakati akiwaeleza maofisa habari na mawasiliano kutoka wizara mbalimbali waliokwenda kuangalia hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa kivuko hicho.

Alisema kazi ya ujenzi wa kivuko hicho imekamilika kilichobaki ni kuweka nyaya za umeme, kupaka rangi pamoja na kuweka viti kwa ajili ya abiria.

Saadun alisema kivuko hicho kinachotengenezwa na kampuni hiyo ya Kijerumani, kina uwezo wa kubeba tani 500 ambapo kitakuwa kikichukua abiria 2,000 na magari 60 kwa wakati mmoja.

Alisema kivuko hicho kimeundwa katika hali inayoruhusu abiria kutumia njia zao katika kuingia ndani na kutoka tofauti na zile za vyombo vya usafiri.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©