Mount Kilimanjaro

 

 

 

Your community website

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

ProfileToolsGamesCommunity

NEWS archive

 
 

 06 January 2008

Gordon Brown aitisha usuluhisho Kenya

Waziri Mkuu wa UK bwana Gordon Brown amewasisitiza viongozi wa Kenya kumaliza machafuko yanayoendelea ambayo yameleta mifereji ya damu ndani ya nchi hiyo.

Bwana Gordon Brown amesema, serikali ya UK inafanya kazi usiku na mchana kusuluhisha machafuko hayo kwa kuwapatanisha viongozi wa serikali ya Kenya. Zaidi ya watu 300 wamefariki mwezi uliopita katika machafuko yaliyoletwa baada ya uchaguzi wa urais ambao ulishindwa na Mwai Kibaki.

Inasemekana hali hiyo inaweza kuzidi kuwa mbaya kwasababu inaelekea kwenye vita vya ukabila.

Bwana Odinga ambaye alikuwa akigombea urais dhidi ya Mwai Kibaki, amekubali wito wa bwana Gordon Brown kukutana na kuzungumzia mapatano kati ya vyama hivyo. Rais wa Ghana John Kufuor, ambaye ni kiongozi wa umoja wa Afrika anatarajiwa katika mazungumzo hayo kuwa kama mmoja wa wasuluhishi.

Watoa huduma wamesema, hali ya watu inazidi kuwa mbaya. Karibu watu 250,000 hawana pa kukaa wala hawana chakula bora.

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
Events Calendar
News Archive 2008
News Archive 2007

External Links

Alnoor CET
TZ Embassy UK
TZ's Community UK

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©