Mount Kilimanjaro

 

 

 

Your community website

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

ProfileToolsGamesCommunity

NEWS archive

 
 

 12 January 2008

Filamu ya Benazir Bhutto (Bhutto The Movie)

Mauaji ya Benazir Bhutto yalikuwa ni drama na yameonekana kwenye televisheni dunia nzima na kwenye vyombo mbalimbali vya habari.

Mpaka sasa, makampuni makubwa ya filamu wanashindania kupata fursa ya kutengenza filamu ya 'Bhutto The Movie'. Vishesh Films na Vox Vision/Sum Films wamesema wameshaanza kukusanya habari za historia ya kiongozi wa zamani wa Pakistan, Benazir Bhutto. Mkurugenzi Mukesh Bhatt wa kampuni ya Vishesh Films iliyopo Mumbai, India, amesema watu maalum wa kutoka chama cha (PPP) cha Benazir Bhutto wamemfuata kuzungumzia fikra hiyo na wamesisitiza watakapoitengeneza filamu hiyo, kufanya haki kwa upande wa Benazir Bhutto. Sehemu za kuchukuliwa filamu hiyo itakuwa Karachi, America, Britain na Dubai alipokuwa akiishi baada ya kuondoka Pakistan kisiasa mwaka 1999.

Inasemekana kuwa marehemu Benazir Bhutto alipoenda kutembea India mwaka 1972, alipewa fursa na kampuni ya Bollywood kuwa katika filamu ya kihindi. Wakati huo alikuwa miaka 18. Kushoto pichani, Benazir Bhutto na waziri wa mambo ya nje wa India walipotembelea India na baba yake marehemu rais Zulfikar Ali Bhutto alipokutana na Indira Gandhi mwaka 1972.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
Events Calendar
News Archive 2008
News Archive 2007

External Links

Alnoor CET
TZ Embassy UK
TZ's Community UK

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©