![]() |
Your community website |
![]() |
||||||
|
|
|
|||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
NEWS archive |
||||||||
|
12 January 2008 |
||||||||
Sherehe za miaka 44 ya mapinduzi ya Zanzibar
JK akiwa ameongozana na mama wa kwanza Bi Salma Kikwete, akigongesheana na mmoja wa maelfu ya watu waliohudhuria sherehe za miaka 44 ya mapinduzi ya Zanzibar katika uwanja wa Amani. Hapo hapo, rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi, Aman Abeid Karume ametoa msamaha kwa wafungwa 25 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 44 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar, kifungu cha 59 kina mpa Rais uwezo wa kutoa msamaha kwa mfungwa yeyote kwa kumuachia kuwa huru au kumpunguzia adhabu. Misamaha kama hiyo imeanza kutolewa na kiongozi wa awamu ya mwanzo marehemu Abeid Amani Karume ambapo ilikuwa kila zifikapo sherehe za Mapinduzi baadhi ya wafungwa waliokuwa wakistahili kwa mujibu wa sheria walikuwa wakipata msamaha. Msamaha huo umewahusisha wafungwa mbalimbali kutokana na vigezo tofauti vikiwemo uzee, maradhi, waliobakisha muda mfupi kumaliza kifungo chao, wanaofuata maadili mazuri, wafungwa wasioweza kufanya kazi kutokana na uzee au ugonjwa na wengineo. Msamaha huo hautawahusu wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa makubwa yakiwemo, waliopatikana na hatia ya biashara ya madawa ya kulevya, unyang`anyi wa kutumia silaha, ubakaji na waliofungwa kifungo cha maisha.
Mapinduzi hayo ndiyo yaliyozaa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Aprili 1964 na kupatikana Taifa la Tanzania chini ya uongozi wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
|
||||||||
|
Custom Search
|
||||||||
|
|
|
|||||||
|
©
www.zenjydar.co.uk - Since 2007 |
|
||||||||