![]() |
Your community website |
![]() |
||||||
|
|
|
|||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
NEWS |
||||||||
|
|
||||||||
Kevin Keegan arudi uwanjani18/01/2008
Kevin Keegan alitambuliwa rasmi na washabiki wake kuwa ni meneja mpya wa timu ya Newcastle United tarehe 17/01/2008. Maongezi ya kumrudisha Kevin Keegan St. James Park, Newcastle, yalichukuwa masaa matatu mpaka kukubaliana kati ya timu ya Newcastle na Kevin Keegan.
Kevin Keegan aliwaambia waandishi wa habari kuwa kazi hii hainitishi kuichukuwa na timu hii hainitishi kuiongoza. Aliendelea kusema, washabiki wanataraji mengi katika timu hii, upinzani mkubwa ambao tunao ni vipi tutaweza kuwapatia wanayoyatarajia. Meneja huyo mpya alisema, atajaribu kuongea na Alan Shearer, ambaye pia alikuwa ni mshambuliaji maarufu wa timu hiyo, kama atataka kufanya nae kazi katika kuindeleza timu hiyo, na kama atataka ataangalia nafasi gani Alan Shearer awe nayo katika kuiongoza timu hiyo.
Keegan, meneja mpya wa Newcastle, atatoka rasmi mbele ya washabiki wake na washabiki wa Newcastle kwenye mechi ya Newcastle na Bolton ambayo itachezwa Jumamosi jioni, tarehe 19/01/2008 katika uwanja wa St. James Park, Newcastle.
|
||||||||
|
Custom Search
|
||||||||
|
|
|
|||||||
|
©
www.zenjydar.co.uk - Since 2007 |
|
||||||||