![]() |
Your community website |
![]() |
||||||
|
|
|
|||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
NEWS |
||||||||
|
|
||||||||
Batman na Robin wa Argos19/01/2008
Kamera ya Zenjydar imemnasa Batman na Robin ambao walikuwa wakichangamsha watu na huku wakigawa toleo jipya la vitabu (catalogues) vya duka la Argos ambalo lipo maeneo ya Beckton, mjini London. Argos ni moja kati ya maduka makubwa ya nchini UK ambayo yanauza bidhaa tofauti za mahitaji ya kila siku. Batman na Robin wametokea kupendwa na watoto kutokana na vitabu vyake vya katuni ambayo inagusia watu hao wawili (Batman na Robin) na kuja kupendwa na watu wazima baada ya kitabu hicho kufanywa kuwa filamu.
Chanzo cha Batman na Robin kama kinavyozungumziwa na mtunzi wa vitabu hivyo, ni Bruce Wayne ambaye ni (Batman) alishuhudia mauaji ya wazazi wake walipokuwa wakiuliwa mbele yake na baadaye kuamua kujiita Batman na kupigana vita na jinai. Na baada ya Dick Grayson ambaye ni (Robin) walipouliwa wazazi wake, Batman alimchukuwa na kumfundisha ustadi wa kupigana vita na jinai. Filamu ya mwisho ya Batman ilitoka mwaka 2005 - Batman Begins. Hollywood (db Techno) Warner Bros. wameshatengeneza filamu mpya ya Batman ambayo inatarajiwa kutoka hivi karibuni, lakini imecheleweshwa kutokana na mabishano na waandishi wa Hollywood ambayo yametokea wiki zilizopita.
Filamu hiyo inaitwa Justice League ambayo muendeshaji filamu hiyo aliitaka iwe katika majumba ya sinema mwanzoni mwa mwaka 2009, lakini kuna uwezekano wa kuchelewa mpaka mwaka 2010 pamoja na filamu mpya ya Superman ambayo ipo matayarishoni.
|
||||||||
|
Custom Search
|
||||||||
|
|
|
|||||||
|
©
www.zenjydar.co.uk - Since 2007 |
|
||||||||