Mount Kilimanjaro

 

 

 

Your community website

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Umoja wa nchi za Ulaya wataka utulivu Kenya

20/01/2008

Baada ya mazungumzo na rais wa Ghana na baada ya mazungumzo na bwana Koffi Annan kushindikana kuhusu vurugu la Kenya, kamati maalum ya nchi za umoja wa ulaya (EU) wamewasili nchini Kenya kuleta utulivu nchini humo. Wamesisitiza kwa pande zote mbili za upinzani kusimamisha uchochezi ambao umesababisha vifo na chuki kati ya wananchi nchini Kenya.

Bwana Louis Michel ambaye anaongoza kamati hiyo ameshawasili nchini Kenya na mpaka sasa ameshaongea na viongozi wa pande zote mbili za upinzani, rais Mwai Kibaki na mpinzani wake wa chama cha ODM, Raila Odinga.

Chama cha Bwana Odinga kilitangaza wazi kuwa watafanya tena maandamano Alhamisi inayokuja ya tarehe 24/01/2008. Maandamano yaliyopita yalisababisha zaidi ya watu 600 kuuwawa na watu 28 kuuwawa siku nne zilizopita.

Katika mkutano huo ambao ulifanyika mjini Nairobi na viongozi wa vyama vyote viwili, bwana Louis Michel aliwaomba vyama vyote viwili kuwashauri polisi wa Kenya kupunguza nguvu ambazo wanazitumia kwa raia wanaoshabikia upinzani na akaongeza kwa kusema, tunaomba utulivu na utulivu uwe wa manufaa ya kuleta maelewano. Hapo hapo alikiomba chama cha upinzani kupunguza maandamano ya mara kwa mara ambayo huwa yanaelekea kwenye vurugu na vifo.

Bwana Koffi Annan anatarajiwa kurudi tena Kenya na kuwepo kwenye mazungumzo hayo ya kuleta utulivu nchini humo.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
Events Calendar
News Archive 2008
News Archive 2007

External Links

Alnoor CET
TZ Embassy UK
TZ's Community UK

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©