![]() |
Your community website |
![]() |
||||||
|
|
|
|||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
NEWS |
||||||||
|
|
||||||||
Virgin Atlantic yazindua dizaini ya 'Spaceliner'23/01/2008
Virgin Galactic ya (Virgin Atlantic) wamezindua dizaini ya ndege ambayo itakayochukuwa abiria kwenda angani kwa matembezi ya utalii. Mwenye kumiliki shirika la ndege hilo bwana Richard Branson, alisema kutangazia waandishi wa habari mjini New York kuwa, ndege hiyo ambayo inategemewa kuanza huduma zake mwaka 2009 (mwakani), itakuwa na ushindani mkubwa katika uekezaji ambao utashinda uekezaji wa simu za mikono na teknolojia ya mtandao ambazo mwanzoni zilikuwa zikitumika jeshini na baadaye kutumika kwa watu binafsi.
Virgin Galactic iliingia mkataba na msanifu maarufu kwa ubunifu wa miundo ya mambo ya anga, bwana Burt Rutan kutengeneza miundo ya ndege za Virgin Galactic, ambazo zitakazochukuwa abiria wa kwenda angani kwa utalii.
Ndege hiyo, itabebwa na ndege nyengine ambayo inajulikana kama (White Knight Two) ambayo itakwenda mpaka itakapofikia kikomo chake itabana mabawa yake na kuiachia ndege itakayobeba abiria (Spaceliner) kufungua mabawa yake na kuongoza kuelekea kituoni. Ndege hiyo itaanza mazoezi yake miezi ijayo ya mwaka huu (2008), ina uwezo wa kubeba marubani wawili na abiria sita. Uwanja wa ndege wake upo katika jangwa la New Mexico, America, ambao unaitwa (Spaceport America). Tikiti ya ndege hiyo kwa kila abiria ni $200,000 (dola laki mbili za Kimarekani) na mpaka sasa watu 200 wameshaagiza tiketi zao na wengine 85,000 wamejisajili kwa tiketi za baadaye.
|
||||||||
|
Custom Search
|
||||||||
|
|
|
|||||||
|
©
www.zenjydar.co.uk - Since 2007 |
|
||||||||