![]() |
Your community website |
![]() |
||||||
|
|
|
|||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
NEWS |
||||||||
|
|
||||||||
Mtoto aliyerushwa kutoka ghorofa ya tatu06/02/2008
Picha ya mtoto aliyerushwa kutoka ghorofa ya tatu na wazee wake huko Ujerumani, ilistaajabisha dunia; na kwa bahati nzuri, mtoto huyo alidakwa na wanazimamoto na yupo katika afya nzuri kabisa.
Wazee wa mtoto Onur Calar (pichani juu) walibanwa kutoka katika jumba walilokuwa wakiishi ambalo lilikamata moto na kusababisha wazee hao kuamua kumtupa mtoto wao dirishani huku wanazimamoto wakiwa tayari chini ya jumba hilo na msitu wa mikono ambayo ilisaidia kumdaka mtoto huyo na kufika kwenye mikono yao salama bila ya kuwa na nyavu wala blanketi.
Tukio hilo si kwa mtoto huyo tu, pia wazazi wengine (wengi wao walikuwa Waturuki) waliokuwamo kwenye jumba hilo waliwarusha watoto wao kwenye mikono ya wanazimamoto na wazazi wengine kuamua kujirusha baada ya watoto wao kusalimika wakiwemo wazee wa mtoto huyo ambao inasemekana bado wapo hospitali na majeraha madogo madogo. Lakini picha ya mtoto (Onur Calar) ndiyo iliyoshtua dunia.
|
||||||||
|
Custom Search
|
||||||||
|
|
|
|||||||
|
©
www.zenjydar.co.uk - Since 2007 |
|
||||||||