![]() |
Your community website |
![]() |
||||||
|
|
|
|||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
NEWS |
||||||||
|
|
||||||||
England 2 - 1 Switzerland = CAPELLO06/02/2008
England 2, Switzerland 1. Goli la kwanza la England limefungwa na Jermaine Jenas katika dakika ya 40, na goli la pili limefungwa na Shaun Wright-phillips katika dakika ya 62. Fabio Capello kashinda mechi yake ya kwanza, lakini je, mashabiki wa timu ya England wajisahau na ushindi huo mmoja? Kihistoria, Meneja sita waliopita waliyoongoza timu ya England katika mechi zao za kwanza walishinda akiwemo Graham Taylor, ambaye alishindwa kuipeleka England kushindana World Cup ya mwaka 1994 iliyofanyika Marekani. Wakati utamu wa ushindi haujaisha na wachezaji kuonyesha machejo na ari uwanjani kwa pasi na kuonana, bado kazi ipo mbele hasa katika kulikimbilia kombe la dunia ambayo michuano yake inaanza mwezi wa tisa mwaka huu.
Steven Gerrard alionyesha maana ya kuwa Kapteni na aliitumia nafasi yake kwa ari na kuonyesha mfano mzuri akiwa kama ni nahodha wa wachezaji wake. Kabla ya michuano ya mwezi wa tisa ya kugombea nafasi ya kwenda Afrika ya kusini mwaka 2010, Capello na kundi lake watarudi tena uwanjani inasemekana mwezi wa tano katika mechi ya kirafiki ya majaribio ya timu yake kwenda Afrika kusini. Na kabla ya mechi hiyo, Wana wa Capello watacheza na France mjini Paris, tarehe 26/03/2008, na kabla ya hapo kunradhi wapenzi wa Uswizi, England na Capello itakuwa ndiyo mechi yao ya kwanza ya kisawasawa kuonyesha nguvu yao mpya chini ya Meneja wao mpya Capello.
|
||||||||
|
Custom Search
|
||||||||
|
|
|
|||||||
|
©
www.zenjydar.co.uk - Since 2007 |
|
||||||||