![]() |
Your community website |
![]() |
||||||
|
|
|
|||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
NEWS |
||||||||
|
|
||||||||
Singapore yafungua gurudumu la kuona mbali02/03/2008
Singapore yafungua rasmi gurudumu la kuona mbali kama lililokuwepo mjini London (the London Eye), Singapore wameliita gurudumu lao (the Singapore Flyer) ambalo limefunguliwa rasmi kwa watalii na wenyeji kulitumia kuuona vizuri mji wao wakiwa angani.
Gurudumu hilo lina urefu wa mita 165 ni sawasawa na jumba lenye ghorofa 42 kwenda juu ambalo ni refu mara 30 kuliko 'the London Eye'.
Sehemu lililowekwa gurudumu hilo, ni sehemu ambayo ufikapo kileleni cha gurudumu hilo unapata kuona sehemu kubwa ya Singapore, pamoja na baadhi ya sehemu za nchi jirani kama Malaysia na Indonesia, kwa mbali.
Watalii na wenyeji wa nchi hiyo wataweza kusanifu mji wa Singapore kwa kuchukua picha za juu (aerial view) wakiwa katika gurudumu hilo kama ionekanavyo pichani juu.
Gurudumu hilo lina vyumba au (kapsuli) 28 vya kuchukulia watu na kila chumba kimoja kinachukua watu 28 kwa mara moja. Gurudumu hilo linachukua takriban dakika 30 mzunguko wake, na 'fee' za kupanda gurudumu hilo ni takriban £10.
The Singapore Flyer, inavyoonekana kwa usiku.
|
||||||||
|
Custom Search
|
||||||||
|
|
|
|||||||
|
©
www.zenjydar.co.uk - Since 2007 |
|
||||||||