![]() |
Your community website |
![]() |
||||||
|
|
|
|||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
NEWS |
||||||||
|
|
||||||||
Ajali ya magari njia ya Dubai na Abu Dhabi11/03/2008
Ajali ya magari zaidi ya mia ambayo yamelundikana na mengine kuungua moto katika ajali iliyotokea katikati ya njia ya Dubai na Abu Dhabi iliyotokea Jumanne ya tarehe 11/03/2008.
Ajali hiyo ambayo imesababishwa na ukungu uliotanda kwenye njia ambao umepunguza uwazi wa kuona mbali chini ya mita 50 ambayo ni sawasawa na nusu kiwanja cha mpira wa miguu.
Ajali hiyo imesababisha magari zaidi ya mia kugongana yakiwemo mabasi yanayochukua wafanyakazi kutoka Abu Dhabi kuelekea bandari ya Jebel Ali ambayo ipo Dubai.
Juu ni ramani inayoonyesha sehemu ambayo iliyotokea ajali hiyo.
Polisi ya UAE imetangaza magari 25 yameshika motomoto baada ya ajali kutokea.
Majeruhi waliwahiwa kwenye hospitali za karibu ambazo zipo na ajali, hospitali mojawapo ikiwemo Mafraq Hospital ambayo ipo Abu Dhabi.
Baadhi ya majeruhi waliowahishwa hospitali.
Walioshuhudia walisema ajali ilikuwa ni 'disaster'; na mlolongo wa magari yalisimama kutembea kwenda njia zote mbili (Abu Dhabi na Dubai).
Wanazimamoto wakiondoa vifusi vilivyosambaratika kutokana na ajali hiyo.
|
||||||||
|
Custom Search
|
||||||||
|
|
|
|||||||
|
©
www.zenjydar.co.uk - Since 2007 |
|
||||||||