![]() |
Your community website |
![]() |
||||||
|
|
|
|||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
|
||||||||
|
NEWS |
||||||||
|
|
||||||||
Ujumbe wa Leo kutoka Dar, "Ya Mungu Mengi"08/04/2008
Pichani juu ni ujumbe wa leo kutoka Dar es Salaam. Bi Bahati Iddi Nzimano
Je, wamkumbuka Bi. Bahati Iddi Nzimano? yule dada wa Tabora aliyezaliwa bila mikono na ambaye amekataa kuwa ombaomba mitaani kutokana na ulemevu wake? basi bahati bado anadunda na pamoja na shida ndogo ndogo za kawaida kwa binadamu yeyote anaendelea na maisha kama kawaida. Hivi sasa yeye ni mjumbe wa taifa wa mkoa wa Tabora katika mkutano mkuu wa chama cha wenye ulemavu nchini na mwaka juzi kwenye uchaguzi mkuu nusura aukwae ubunge kupitia viti maalumu vya wenye ulemavu, lakini bahati haikuwa yake aliambulia kuwa mtu wa tatu. Bi Bahati alitembelea Dar es Salaam hivi karibuni katika ziara yake ya kikazi na Kaka Michuzi alipata bahati ya kutembelewa ofisini kwake na Bi Bahati ambako hakusita kumuonesha namna anavyoweza kumudu maisha kwa kutumia miguu (kwa kupiga simu ya mkononi kwa kutumia miguu) na mengineyo.
Bado tu hujaamini...
|
||||||||
|
Custom Search
|
||||||||
|
|
|
|||||||
|
©
www.zenjydar.co.uk - Since 2007 |
|
||||||||