Mount Kilimanjaro

 

 

 

Your community website

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

China yajitayarisha kukabiliana na Olimpik ya 2008

12/04/2008

China inaandaa kikosi maalum cha kukabiliana na Olimpik itakayofanyika mjini Beijing mwaka huu 2008.

Kutokana na wakuu wa ulinzi wa Uchina, kikosi hicho kimeandaliwa kukabiliana na ujinai, ugaidi, uvurumi na mengine yanayohatarisha usalama wa raia na watakaohudhuria Olimpik kwa ujumla.

Polisi wa kikosi maalum wakihusishwa katika mazoezi mbalimbali ya kila siku kuwa tayari na pirika zozote zitakazotokea.

Hapo juu pichani siyo filamu ya kiini macho, hapo ni mikono kavu-kavu

Polisi hao wanafanya mazoezi nchi kavu na ufukoni mwa bahari iwapo kutatokea chochote cha hatari kwa njia ya bahari ambacho si cha kutegemewa.

Pichani, mmoja wa polisi akionekana akimpa maelekezo Ng'ang'a wake jinsi ya kukabiliana na ugaidi. Inasemekana timu hii itachukuwa nafasi kubwa kwenye maeneo yanayozunguka matukio la Olimpik hasa viwanja vya mpira wa miguu.

Beijing hivi sasa, ulinzi umekuwa jambo aula baada ya mambo yaliyojitokeza hivi karibuni kuhusu Tibet.

 

Kikosi maalum kikifanya mazoezi kwenye theluji (snow) kwa kupakaza barafu kwenye mwili kuonyesha ukakamavu wa mwili.

Kikosi hicho kinaonyesha mbinu za kukabiliana nchi kavu na ndani ya maji.

KUNG FU imezaliwa China

Kikosi cha ulinzi kikifanya mazoezi ya kukabiliana na washabiki wa mpira wa miguu na yoyote yule mwenye kuleta fujo.

Kikosi hicho kimetengewa sehemu maalum katika ziwa la Wuhan, China, kwa mazoezi ya kukabiliana lolote litakalotokea kwa njia ya maji.

Inasemekana, katika kikosi hichi, watu 600 ziada wameandikishwa iwapo kutatokea na mafuriko bila ya kutarajiwa.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
Events Calendar
News Archive 2008
News Archive 2007

External Links

Alnoor CET
TZ Embassy UK
TZ's Community UK

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©