Air Tanzania yapewa mbawa
na Serikali
04/01/2009

Serikali
imetoa Sh. bilioni 2.5 kwa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) ikiwa ni
fedha za awali za kuendesha kampuni hiyo na kulipa baadhi ya madeni kati
ya Sh bilioni 3.3 zilizoombwa na kampuni hiyo kama mtaji wa haraka.
Sambamba
na hilo, Waziri wa Maendeleo ya Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa
ameunda Tume na kuitaka ifanye kazi kwa siku 21 tangu Desemba 29, mwaka
jana ili kubainisha kiini cha matatizo ya ATCL baada ya ripoti ya Bodi
ya kampuni hiyo kutotoa maelezo ya kutosheleza.
Mwenyekiti wa Tume hiyo ya watu saba ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha
Ardhi, Profesa Idrissa Mshoro na wajumbe wengine sita, alisema hayo Dk.
Kawambwa.
Kuhusu
mtaji huo wa Sh bilioni 2.5, Dk. Kawambwa aliwaambia waandishi wa habari
jana Dar es Salaam kuwa serikali imeamua kuibeba ATCL kuanzia mtaji
mpaka ulipaji wa madeni kwa kuwa ni mmiliki wa kampuni hiyo na kwamba
itatoa fedha kwa awamu kulingana na mahitaji ya wakati ya kampuni hiyo.
|