Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Mashindano ya usanifu wa basi jipya la LONDON

06/01/2009

Baada ya mamlaka ya London kuamua kutangaza mashindano ya kusanifu uchoraji wa mabasi mapya ambayo yatahudumia wakazi na watalii wa London katika jitihada za kubadilisha mabasi maarufu yaliyopo hivi sasa ambayo yakijulikana kama (London Bus au Red Bus au Double Decker au Routemaster), vigogo vya usanifu walioshiriki katika mashindano hayo yaliyoitwa "Imagine a bus for London", wamejipinda na kujipindua kuleta ufanisi wa sura mpya ya mabasi hayo ambayo yatabadilisha uso wa mitaa ya London.

Mashindano hayo yalikuwa katika aina nne za washindani. Washindani wa umri chini ya miaka 11, 11-16, 16-18 na 18 na zaidi.

Maombi 475 ya washindani yalipokewa kutoka sehemu mbalimbali za UK.

Washiriki waliombwa wabuni mabasi ambayo yatashabihi miundo ya karne mpya (21st Century) kikamilifu kila pembe kwa utondoti na kwa yule atakayefaulu kaahidiwa ubunifu wake utachukuliwa kwenye kiwanda kikubwa kilichotayarishwa cha kutengeneza mabasi mapya ya London ambapo sura hiyo itabidilishwa kutoka kwenye picha kuwa basi hai.

Picha nyingi zilizoingia kwenye mashindano hayo ni picha mbili tu zilizoshinda kwa kuchukuwa nafasi ya kwanza. Washindi waliosanifu picha hizo wamezawadia £25,000 kila mtu na ubunifu wa ndio utakaochukuliwa kutengenezwa mabasi mapya ya London.

Mshindi wa Kwanza: Alan Ponsford (57) wa Capoco Design Limited, UK. £25,000.

Mshindi mwingine wa Kwanza: Aston Martin and Foster + Partners, London. £25,000.

Mshindi anayefuata: Hector Serrano Studio na Minarro Garcia wa (UK na Spain). £10,000.

Mshindi anayefuata: Jamie Martin, UK. £10,000.

Mshindi anayefuata: LA:UK Design Ltd, UK. £2,000.

Mshindi anayefuata: Concrete All Round Creative, Belgium. £2,000.

Mshindi anayefuata: Lotti Duke, UK. £1,000.

  • Mabasi mapya ambayo yatatengenezwa kufuatia ubunifu wa mshindi wa kwanza Capoco, yataendeshwa kwa kutumia Hydrogen (kwa nguvu ya umeme) badala ya kutumia Diesel.

  • Yatakuwa na viti vya ziada vya watu wanne (4) zaidi ya mabasi ya zamani na ukumbi wa watu thelathini (30) wa kusimama wima.

  • Dereva na Kondakta watawasiliana kwa kutumia vifaa vya kupaza sauti visivyo na waya (wireless headsets).

  • Gharama ya mabasi mapya yanatarajiwa kugharimu £150,000.

Routemasters zikionekana zikiwa katika mtaa wa Oxford Street, London, 1947.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©