Bi Sophia Simba achaguliwa
kuwa mkuu wa UWT
10/01/2009

Bibi Sophia Simba ameibuka kinara na
kuchaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT).
Sophia ambaye kitaaluma ni mwanasheria aliyehitimu kutoka vyuo vikuu vya
Dar Es Salaam (Shahada ya kwanza) na chuo kikuu cha Zimbambwe (diploma
ya uzamivu), alimshinda mpinzani wake mkubwa, Bi Janeth Kahama. Kwa
ushindi huo Bibi Sophia Simba anachukua mikoba ya uongozi wa chama hicho
kutoka kwa Bibi Anna Abdallah aliyeongoza umoja huo kwa takriban miaka
15.
|