Dala dala yateketea kwa
nguvu ya umeme
11/01/2009

Wapita
njia wakiliangalia basi la abiria aina ya DCM lililoteketea kwa moto
baada ya kuacha njia na kugonga nguzo za umeme zenye Transfoma na
kusababisha mlipuko karibu na kituo cha daladala Banana, Ukonga, Dar es
Salaam.
Ajali
hiyo iliyotokea jana usiku haikuleta madhara kwa abiria waliokuwemo
ndani ya basi hilo.

Pichani
mafundi umeme wa Shirika la Ugavi wa Umeme Nchini (TANESCO) wakiondoka
eneo la tukio baada ya kuangalia athari iliyotokea baada ya ajali hiyo.
Eneo la Banana litaendelea kuwa gizani kwa kipindi kisichojulikana mpaka
itakapofungwa transfoma nyingine kutokana na Transfoma iliyokuwa
ikifanya kazi kuungua.
|