Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Jaji Mkuu aapisha maofisa wapya

15/01/2009

Jaji mkuu wa Tanzania Agustino Ramadhan akimwapisha Bw. John Mgeta kuwa Kaimu Naibu Msajili wa Mahakama Rufani Tanzania leo katika ukumbi wa mahakama ya rufaa Tanzania jijini Dar es salaam. Upande wa kulia wa jaji mkuu ni Kaimu jaji kiongozi kanda ya Dar es salaam Aristoclas Kaijage.

Bw. Huruma Shaidi akipeana mkono na Jaji Mkuu wa Tanzania Agustino Ramadhani mara baada ya kuapishwa na kupokea hati ya uteuzi kuwa Kaimu Naibu Msajili wa Mahakama kuu, Kitengo cha Biashara Mwanza leo jijini Dar es Salaam.

Jaji mkuu wa Tanzania Agustino Ramadhan akipeana mkono na Bi. Happines Ndesamburo mara baada ya kuapishwa kuwa Kaimu Naibu Msajili wa Kitengo cha Biashara Mahakama kuu kanda ya Arusha katika sherehe fupi iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mahakama ya Rufaa jijini Dar es salaam.

Jaji Mkuu wa Tanzania Agustino Ramadhan (mstari wa mbele katikati) katika picha ya pamoja na maofisa wa mahakama (waliosimama mstari wa nyuma) mara baada ya sherehe fupi ya kuwaapisha kushika nyadhifa mbalimbali leo jijini Dar es salaam.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©