Chelsey Sullenberg, pichani, ni rubani wa
shirika la ndege la US Airways ambaye alithibitisha kuwa ni kapteni na
shujaa wa ndege aina ya Airbus 320 namba 1549 iliyoruka kutoka uwanja wa
ndege wa LaGuardia uliopo New York kuelekea mji wa Charlotte, North
Carolina siku ya Ijumaa ya tarehe 16/01/2009.
Ushujaa wake ulikuja baada ya kuishusha
ndege hiyo kwenye mto wa Hudson uliopo Manhattan, New York, mara baada
ya kupatwa na ajali na kuokoa maisha ya watu wote 155 waliomo ndani ya
ndege hiyo.
Bwana Chelsey ana uzoefu wa kurusha ndege
za abiria usiopungua miaka 29 na kabla ya hapo alikuwa rubani wa ndege
za kivita za US Airforce.
Mara baada ya kuruka uwanja wa ndege wa
LaGuardia, bwana Sullenberg alihisi tofauti ya mwenendo wa ndege yake na
mwisho kutambua kuwa injini zote mbili za ndege zilikuwa zipo katika
hali ya utata na isitoshe moja ilikuwa ishaanza kuwaka moto.
Uwanja wa ndege wa karibu wa kuitulisha
ndege hiyo ulikuwa mbali naye na hakuwa na khiyari bali kuishusha ndege
hiyo kwenye maji ya mto wa Hudson (Hudson River), magharibi mwa mji wa
Manhattan.
Mara baada ya kutua salama na kuokoa watu
wote waliokuwamo kwenye ndege hiyo, bwana Sullenberg alitembea kutoka
jikoni alipo mpaka kwenye mkia wa ndege kuhakikisha watu wote wametoka
kwa usalama na hakujabaki mtu ndani ya ndege hiyo.
Inasemekana ajali hiyo ilisababishwa na
ndege wakubwa aina ya bata warukao angani kuingia kwenye injini ya ndege
mnamo saa 3.26pm sekunde 30 au 45 baada ya kuruka tu kutoka uwanjani.
Shujaa huyo kapongezwa na viongozi mbalimbali wa nchini Marekani katika
sakata hilo lililoitwa "Miracle on the Hudson".
Mawasiliano baina ya Rubani na muongoza njia za hewa bonyeza hapa chini.
Angalia filamu iliyotengenezwa hai ya tukio hilo kwa kubonyeza hapa
chini.
Angalia filamu ya kweli iliyokamatwa na CCTV ya Coast Guard kwa
kubonyeza hapa chini.