Barack Obama achukua kiapo
kwa mara ya pili
21/01/2009

Jumatano ya tarehe 21/01/2009, Jaji Mkuu,
John G. Roberts Jr. akimuapisha rais Barack Obama kwa mara ya pili ndani
ya ikulu (White House, Map Room).
Kiapo hicho kimekuja baada ya kiapo cha
kwanza cha rais kuwamo kwenye midomo ya wengi kwa kugeuzwa sentensi ya
kiapo hiko kwa bahati mbaya.
Kiapo hiki Bwana Roberts alianza na
kumuuliza Barack Obama kama yuko tayari kuchukua kiapo kwa mara ya pili,
Barack akamjibu, "I am, and we're going to do it very slowly".
Kiapo hichi hakikubatilisha Barack Obama
kuwa rais wa 44 wa Marekani siku ya Jumanne ya tarehe 20/01/2009 kama
katiba inavyosema ikiingia saa sita mchana tu, aidha kaapishwa au
hajaapishwa tayari ameshakua rais wa Marekani.
|