Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Teknolojia mpya ya Google map

29/01/2009

Kampuni kubwa ya mtandao duniani (GOOGLE) imezindua teknolojia mpya ya kuchambua mitaa ya UK kwa wanaotumia Google map kupata picha halisi ya sehemu za UK uso kwa macho ukiwa katika kiti cha kompyuta yuko.

Teknolojia hiyo ambayo inaitwa "Street View" inakupa sura ya mitaa ya UK pembe zote (360 degree) kama ukiwepo sehemu hiyo hai.

Mtu yoyote ambaye yupo popote duniani akiandika anuani au 'post code' ya mahali pa London anaweza kupata picha halisi ya anuani hiyo na kumuezesha kuona nyumba, magari, watu na kila kitu kama vile yupo pale yeye mwenyewe hai na inakuezesha kuangalia sehemu hiyo pande zote (36 degree). Kwa sehemu ambazo hazijatiwa kwenye Google Map, Street View, zinatarajiwa kutiwa siku za mbele.

Watu wataweza kutembelea Big Ben, Tower Bridge, London Eye bila ya kutoka nyumbani kwa kutumia teknolojia hiyo.

Kuangalia inavyofanya kazi, bonyeza hapa na jaribu kuandika anuani upate picha halisi ya sehemu.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©