Mtoto aliyetoweka Tanga
apatikana Dar es Salaam
30/01/2009

Familia
ya mtoto Mbarouk H. Masoud ambaye alitoweka nyumbani kwao huko Mikanjuni,
Tanga tangu Jumatatu 26/01/2009 bila taarifa yoyote, inayo furaha ya
kuwajulisha kuwa mtoto wao Mbarouk Masoud amepatikana huko Dar es Salaam
tarehe 29/01/2009 akiwa salama.
Bado
haijajulikana sababu za mtoto kuondoka kwao bila ya kuaga na hilo
linafanyiwa kazi kifamilia. Familia inashukuru kwa msaada mkubwa
walioupata kutoka kwa ndugu, marafiki, jamaa na taasisi mbalimbali
walioshiriki katika kumtafuta mtoto wao bila kuchoka hadi alipopatikana.
|