Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Wasanii wa UK kuupanda mlima Kilimanjaro

03/02/2009

Wasanii wa fani mbalimbali wa UK wamejitolea mchango wa kusaidia matatizo mbalimbali yanayowakuta watoto na baadhi ya jamii barani Afrika.

Wasanii hao ambao wamepewa fursa na kampuni ya BT (British Telecom) kwa kujitolea kwa njia ya mradi wa COMIC RELIEF kuupanda mlima wa Kilimanjaro, Tanzania kuonyesha nia yao ya kusaidia kukuza mfuko wa msaada uliokusudiwa.

Baadhi ya misaada kusudiwa ikiwamo kupigana vita na magonjwa ya Malaria ambayo inaua wengi barani Afrika kutokana na kuto kuwa na kinga (kama vyandarua na madawa).

Watakaoshiriki kuupanda mlima Kilimanjaro ni kama wafuatao:

Alesha: Muimbaji, mwandishi wa nyimbo, mtangazaji wa TV, mchezaji dansa.

Ben: Mtangazaji wa TV wa Channel 4 UK, na kapata umaarufu wake mkubwa hivi karibuni kwenye kipindi cha X-Factor.

Cheryl: Muimbaji wa kikundi cha Girls Aloud, na kapata umaarufu wake mkubwa hivi karibuni kwenye kipindi cha X-Factor. Cheryl kaolewa na mchezaji maarufu wa England, Ashley Cole ambaye pia ni beki tatu wa timu ya Chelsea.

Chris: DJ wa radio na vilevile ni mtangazaji wa TV.

Denise: Mtangazaji wa TV na muigizaji wa michezo mbalimbali kwenye salasila za TV, UK.

Fearne: Mtangazaji wa TV, na kapata umaarufu wake mkubwa hivi karibuni kwenye kipindi cha X-Factor.

Gary: Muimbaji.

Kimberley: Muimbaji wa kikundi cha Girls Aloud cha UK.

Ronan: Muimbaji wa kikundi cha Boyzone cha UK.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©