Rais Jintao ahitimisha
ziara yake ya Tanzania
17/02/2009

Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete
akimtambulisha Mwenyekiti wa Chama cha CUF Profesa Ibrahim Lipumba kwa
Rais wa China Hu Jintao wakati wa dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa kwa
heshima ya Rais huyo wa China Ikulu jijini Dar es Salaam.

JK akimtabulisha mwanaye Khalfan Kikwete (8) kwa Rais Hu
Jintao wa China muda mfupi kabla ya Rais huyo kutoa mhadhara katika
ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Baadaye Rais huyo
aliondoka nchini baada ya ziara yake ya kikazi ya siku tatu.

Ndege iliyombeba Rais Hu Jintao wa China na ujumbe wake
ikiruka katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere baada ya Rais
huyo kumaliza ziara yake ya kikazi ya siku tatu nchini Tanzania.
|