ZANTEL yafungua tawi Dar
es Salaam
02/03/2009

Shirika la simu za mikono ZANTEL imefungua duka la kisasa
jijini Dar es Salaam katika kuhakikisha upatikanaji wa huduma za shirika
hilo ni wepesi. Duka hilo (pichani) liko katika jengo la Hadi
Apartments, lililopo katikati ya Jiji katika makutano ya Mtaa wa
Morogoro na Libya eneo la Kisutu. Mstahiki Meya wa Jiji la Dar Es Salaam
Alhaji Adam Kimbisa alikuwa mgeni rasmi siku ya ufunguzi wa duka hilo.
|