Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Waziri Mkuu Mizengo Pinda atembelea London

03/03/2009

Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda (aliyekaa watatu kutoka kulia), alikutana na Viongozi wa Jumuia mbalimbali mjini London katika ziara yake ya kikazi. Alipokelewa rasmi na Mheshimiwa balozi wa Tanzania nchini UK, Mwanaidi Maajar (aliyekaa watatu kutoka kushoto). Matembezi hayo yalikuwa kuwashajiisha viongozi wa jumuia mbalimbali katika jitihada zao za kimaendeleo za jumuia za Kitanzania zilizopo nchini UK. Kabla ya matembezi ya mjini London, Mheshimiwa Waziri aliwatembelea jumuia za Northern Ireland.

Mheshimiwa Mizengo Pinda na Mheshimiwa Balozi Mwanaidi Maajar (Waliokaa) wakiwa kwenye picha na Maafisa wakuu wa ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza ambapo Mheshimiwa Waziri Mkuu alitembelea na kukutana nao kuwapongeza na kuwashajiisha kwa kazi ya jitihada za kuwahudumia Watanzania nchini UK.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda (kushoto pichani) akiwalaki Naibu Balozi wa Ubalozi wa Tanzania nchini UK, Mh. Ghabaka Kilumanga na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mh. Mwanaidi Majaar (katikati) nje ya ubalozi huo Tanzania House mjini London.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©