TANESCO na uamuzi wa
mitambo ya DOWANS
08/03/2009

Mkurugenzi mtendaji wa TANESCO, Dk. Idris Rashid
akiwasili kuongea na vyombo vya habari jana makao makuu ya shirika hilo
huko Ubungo, Dar es Salaa, ambapo Dk. Rashid alitangaza uamuzi wa
kujitoa kwa shirika hilo katika nia ya kununua mitambo ya kufua umeme ya
Dowans.
Uamuzi huo umefikiwa baada ya kutolewa taarifa alizodai
kuwa ni za uongo na zilizojaa utashi wa kisiasa zaidi dhidi ya utaalamu
wa TANESCO na kwamba zimechangia kuvunja nguvu ya mamia ya wafanyakazi
wa shirika hilo wanaofanya kazi usiku na mchana kuhakikisha nchi inapata
umeme wa uhakika.

|